MAISHA YA UKRISTO NI ENDELEVU

NA ADELADIUS MAKWEGA

WAKRISTO wametakiwa kulisoma neno la Mungu, kulichukua katika maisha yao na kuliishi huku kila Mkristo akitakiwa kuwa shuhuda kama Yohane Mbatizaji katika maisha yake yote.

Hayo yamesemwa katika misa ya Jumapili ya pili ya mwaka A wa Kanisa, Januari 15, 2023 katika Kanisa la Bikira Maria imakulata, Parokia ya Chamwino Ikulu, Jimbo Kuu Katoliki la Dodoma.
Akihubiri katika misa hiyo, Padri Paul Mapalala amesema kuwa maisha ya Ukristo ni maisha endelevu, siyo muumini akitoka kanisa basi na maisha yake ya Ukristo yanasalia huko huko, hilo hapana, ni lazima kila mmoja awe shuhuda kwa wale ambao hawalisikii neno la Mungu.

“Kama muumini haufanyi hivyo, basi wewe haufai kuwa mfuasi wa Kristo, lazima huyo Kristo ashuhudiwe katika maisha yako ya kila siku popote Mkristo alipo, kama wewe ni mtoto au mtu mzima, iwe nyumbani au kazini, hilo neno jema lipelekwe huko.”

Misa hiyo iliambatana na maombi kadhaa na mojawapo ni hili, “Mungu Baba utasaidia kushuhudia huruma ya Kristo hili kuwasaidia wengine wenye shida za roho na za mwili."

Wakati wa matangazo ndani ya misa hiyo Muuguzi Mkuu Christina Matias aliwaambia waamini kuwa shirika la United Missionaries ambalo huwa linahudumia wakimbizi litaanza utoaji wa chakula kwa wakazi wa Chamwino kuanzia 2023 hadi 2028.

Hadi wakati misa hiyo ya pili ya dominika hii inakamilika hali ya hewa ya eneo la Chamwino ikulu imekuwa ikipata mvua na jua , huku mazao ya wakulima wengi yakiendelea vizuri na wengine wakiendelea na upandaji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news