Benki ya Afrika yakabidhi msaada wa pikipiki Jeshi la Polisi



Mkuu wa Dawati la Jinsia na watoto Naibu Kamishna wa Polisi DCP Maria Nzuki kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IJP Camillus Wambura, Machi 11, 2023 amepokea pikipiki tano aina ya TVS kutoka kwa Benki ya Afrika (Bank of Africa), ambazo zimetolewa kwa lengo la kusaidia ulinzi na usalama katika kata tano za Wilaya ya Chamwino.


DCP Nzuki ameishukuru Benki ya Afrika kwa msaada huo wa pikipiki uliotolewa na benki hiyo ambapo itasaidia kurahisisha kutoa huduma kwa wananchi na kuzidi kuimarisha usalama wa raia na mali zao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news