Mama Mariam Mwinyi ateta na Binti wa mtawala wa zamani wa Qatar


Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi, Mama Mariam Mwinyi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora amekutana na Binti wa mtawala wa zamani wa Qatar, Sheikha Alanoud Hamad Al-Thani jijini Doha, Qatar.

Katika kikao hicho kwa pamoja walibadilishana mawazo juu ya ustawi wa wanawake na vijana hususani wanawake katika kujiendeleza kiuchumi, afya na elimu.

Sheikha amempongeza mama Mariam Mwinyi kwa kuanzisha Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora ambayo imekuwa inapambana na unyanyasaji na ukatili wa kijinsia pamoja na kumwezesha mtoto wa kike katika masuala ya afya ya uzazi, kuwawezesha pia wanawake wanaojishughulisha na ukulima wa mwani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news