Mama Mariam Mwinyi atoa wito kwa Diaspora

NA MWANDISHI WETU

MKE wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi, Mama Mariam Mwinyi,amewasihi wanadiaspora wanawake waishio nchini Qatar kuendeleza utaratibu wao wa kuleta mchango na shukrani nyumbani. Aidha, Mama Mariam Mwinyi amebainisha umuhimu wa kuwasaidia wanawake Zanzibar.
Mama Mariam Mwinyi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora ametumia nafasi hiyo kuwahutubia wanadiaspora wanawake walioko Qatar wakati wa sherehe za kutimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa taasisi yake. 
Sherehe hizo zilifanyika Mei 22, 2023 jijini Doha, Qatar ambapo Mama Mariam Mwinyi ametoa wito kwa wanawake hususani wanadiaspora waishio Qatar, kuwa makini katika malezi ya watoto. 

Wito huo unakuja kufuatia kuongezeka kwa kasi kwa wimbi la udhalilishaji, ambalo kwa kiasi kikubwa linaanzia katika ngazi ya familia.
Pia amesisitiza umuhimu wa kina mama kuwa mstari wa mbele kuchukua hatua za mapema za kuzuia udhalilishaji na amewasihi wanawake hao kujenga mazingira salama na kuhakikisha watoto wanapata malezi bora. 
Kwa upande wa wanadiaspora wamemuhakikishia Mama Mariam Mwinyi kuwa wataendelea kushirikiana naye katika jitihada zake za kuwahudumia wanawake, vijana na watoto nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news