Rais Dkt.Mwinyi atoa wito kwa waandishi wa habari nchini

NA DIRAMAKINI

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema vyombo vya habari vinaweza kutoa mchango mkubwa endapo waandishi wa habari watazingatia uzalendo, weledi na maadili ya taaluma kinyume chake inaweza kufifisha jitihada za maendeleo, kuhatarisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa. 
Rais Dkt. Mwinyi amewataka waandishi wa habari watambue kuwa hakuna uhuru usio na mipaka, wala hakuna uhuru bila wajibu hivyo kwa kuadhimisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari ni muhimu kutambua uzalendo wa nchi.

Ameyasema hayo leo katika siku ya mwisho ya Kongamano la Miaka 30 ya Uhuru wa vyombo vya Habari katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Airport, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Aidha, Rais Dkt.Mwinyi ametoa wito kwa waandishi wa habari watumie fursa ya siku hii kuweka mkazo katika uhuru wa kujieleza ndani ya ajenda ya jumla ya haki za binadamu.

Vilevile, amewataka jumuiya na wadau mbalimbali wa vyombo vya habari watumie siku hii kusherehekea na kuungana na mashirika yanayotangaza masuala ya mazingira, haki za wanawake, haki za watoto, haki za asili, haki za kidijitali, vita dhidi ya ufisadi na mengineyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news