RC Senyamule amjulia hali mama anayesadikiwa kumwagiwa tindikali

NA MWANDISHI WETU

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Mheshimiwa Rosemary Senyamule amemtembelea na kumjulia hali,Bi. Witness Mkuvalwa (mkazi wa Iringa) anayesadikiwa kumwagiwa kimiminika chenye kemikali na kulazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa uangalizi na matibabu.
Senyamule amemtembelea, Bi. Witness leo Juni 30,2023 na kuahidi kushirikiana na Vyombo vya Ulinzi na Usalama vya Mkoa katika kuhakikisha anayetuhumiwa kuhusika na kitendo hicho anachukuliwa hatua na majeruhi wa tukio hilo anapata haki yake.

Kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Dkt. Baraka Mponda amekiri kumpokea Bi.Witness Mkuvalwa jumatano ya Juni 28 mwaka huu ambapo tukio la kumwagiwa kimiminika hicho lilitokea katika Stendi kuu ya Mabasi ya Nanenane jijini Dodoma. 

Katika kuhahikikisha Bi. Witness anarejea katika hali yake ya kawaida madaktari bingwa wa macho,pua, koo na ngozi wamempima mgonjwa huyo na kuthibitisha hakupata madhara makubwa hivyo ataendelea vizuri kutokana na Matibabu anayopatiwa. 

Mhe.Senyamule pia alipata fursa ya kuwatembelea wagonjwa wengine katika wodi mbalimbali wakiwemo majeruhi wa ajali ya Moto waliolazwa katika Hospitali hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news