Chuo Kikuu Mzumbe wahimizwa kuchangamkia fursa urasimishaji biashara kutoka BRELA

MOROGORO-Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), imeitaka jumuiya ya Chuo Kikuu cha Mzumbe kuchangamkia fursa ya kurasimisha biashara zao ili ziweze kutambulika na kulindwa kisheria.
Hayo yamesemwa na Bi. Loy Mhando Mkurugenzi wa Miliki Ubunifu kutoka BRELA wakati akiwasilisha mada kwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu, juu ya umuhimu wa kurasimisha biashara katika Maadhimisho ya Siku ya Mzumbe na Kambi ya Ujasiriamali 2024. Maadhimisho hayo yanayofanyika Chuo Kikuu cha Mzumbe Kampasi Kuu Morogoro kuanzia tarehe 20 hai 22 Machi 2024.

“Zipo faida nyingi zitokanazo na kurasimisha biashara ikiwemo, urahisi wa kufikiwa kwa huduma mbalimbali kwa kuwa kutawezesha kupata takwimu sahihi za biashara, vilevile biashara hizo zitatambulika kisheria. Vilevile, mfanyabishara ataweza kuweka hesabu vizuri na kuweza kupata huduma mbambali ikiwemo ikiwemo mikopo,”alisema Bi. Mhando.

Aidha,Bi. Mhando ameongeza kwa kusema kuwa, urasimishaji biashara utawezesha wafanyabiashara kulipa kodi ambayo itachangia katika kukuza uchumi wa taifa utakaowezesha ujenzi wa miundombinu ya kuwafikia wafanyabiashara sambamba na ujenzi wa masoko na uwekaji wa mazingira wezeshi ya biashara.
Naye Bw. Iddi Mohamed mwanachuo wa mwaka wa pili katika Chuo hicho ameeleza kuwa, amefurahishwa na elimu iliyotolewa na BRELA na kueleza kuwa, awali alikuwa na mawazo ya kuanzisha biashara yake lakini hakufahamu nini afanye, baada ya kupata elimu ya urasimishaji kutoka BRELA amepata uelewa kuwa ukisajili kampuni yako au kurasimisha biashara kwa ujumla, unapata ulinzi wa kisheria na ikitokea changamoto yoyote inakuwa rahisi kukabiliana nayo.
Katika Maadhimosho ya Siku ya Mzumbe na Kambi ya Ujasiriamali 2024, BRELA imeshiriki kwa kutoa mafunzo maalumu juu ya namna ya kurasimisha biashara na kulinda bunifu wanazozifanya sambamba na kutoa huduma ya usajili wa papo kwa papo kwa wanafunzi, wahadhiri na wafanyabiashara waliotembelea katika Maadhimisho hayo.
Maadhimisho hayo yaliyobeba Kauli Mbii isemayo “Kuzingatia Teknolojia Zinazoibukia na Njia Mpya za Kujifunza kwa ajili ya Ukuaji Endelevu”, yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 22 Machi, 2024. Kauli Mbiu hiyo inayolenga kuibua vipaji na mawazo bunifu ya wanafunzi wa Chuo hicho na pia kutoa nafasi kwa wafanyakazi na wanafunzi kuonesha ubunifu walionao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news