Balozi Kasike ateta na Balozi Donat jijini Maputo

MAPUTO-Aprili 2,2024, Mhe. Phaustine Kasike ambaye ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji alitembelewa na Mhe. Ndamage Donat, Balozi wa Jamhuri ya Rwanda nchini Msumbiji.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Aprili 3,2024 na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Maputo,Msumbiji.

Mhe. Balozi Donate alifika kwenye Ubalozi wa Tanzania jijini Maputo kujitambulisha kufuatia kuteuliwa hivi karibuni na nchi yake kuiwakilisha nchini Msumbiji.
Katika Mkutano huo, Viongozi hao wawili walikubaliana kushirikiana kutekeleza majukumu yao kwa maslahi ya nchi zao mbili, ambazo pia ni miongoni mwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zenye uwakilishi nchini Msumbiji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news