DCEA, TAKUKURU wafikisha elimu kwa wanafunzi Chuo cha Afya Mpanda

KATAVI-Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Nyanda za Juu Kusini kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wametoa elimu kwa wanafunzi wa Chuo Cha Afya cha Mpanda kilichopo mkoani Katavi. 
Katika semina hiyo takribani wanafunzi 320 na walimu 12 walipatiwa elimu juu ya madhara yatokanayo na biashara na matumizi ya dawa za kulevya pamoja na rushwa.
Pia, walielezwa wajibu wao kama wataalamu wa afya katika kuhakikisha ustawi wa jamii na kuepuka uchepushaji wa dawa tiba zenye asili ya dawa za kulevya.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news