Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Juni 9,2024

ARUSHA-Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Paul Makonda amemuagiza Mkuu wa Polisi wa Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kutokamata magari ya utalii kwenye mkoa huo na badala yake ukaguzi kwa watalii ufanyike kwenye mipaka na kwenye viwanja vya ndege vinavyotumika na watalii ili kuepusha usumbufu.
Ameyasema hayo mbele ya waandishi wa habari Juni 8, 2024 kwenye Viwanja vya Magereza Kisongo kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya Karibu Kili Fair 2024, yanayojumuisha makampuni zaidi ya 700 ya kimataifa kutoka kwenye mataifa zaidi ya 50. "Kama Serikali ya Mkoa tumeona tuweke mazingira bora zaidi ya kuhakikisha kwamba mtalii anapokuja kwenye mkoa wetu hapati changamoto na ajisikie kuheshimika kwa sababu Taifa limejiandaa kupokea watalii, kuanzia tarehe moja mwezi wa saba tumekubaliana kwamba hakuna polisi kusimamisha gari la utalii.”
















Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news