Nitawapa kila kitu ila kadi ya CCM sitawapa-Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete

MOROGORO-Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze amewaasa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukipigania chama chao kwa wivu mkubwa ili kulinda na kutekeleza malengo ya chama katika kuwahudumia wananchi na kuleta maendeleo kwa wananchi bila ubaguzi.
Mhe.Ridhiwani aliyabainisha hayo mkoani Morogoro wakati akihutubia Mkutano wa Kuwaaga Wanachama wa CCM Seneti ya vyuo na vyuo Vikuu uliofanyika katika chuo cha Mtakatifu Jordan mkoani humo.
"Hata kama ikifika siku chama hichi kinaona Ridhiwani hafai kuwa mwanachama wakaamua kunifukuza nitawapa kila kitu lakini kadi ya Chama cha Mapinduzi sitatoa kwasababu Chama cha Mapinduzi kipo moyoni mwangu na huu ndio msingi ambao mnatakiwa muwe nao,piganieni chama chenu msisubiri kukumbushwa jukumu hilo," alisisitiza Mhe. Ridhiwani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news