Rais Dkt.Samia amwaga shilingi bilioni 45 kutatua tatizo la maji jijini Dodoma

DODOMA-Waziri wa Maji, Mheshimiwa Jumaa Aweso amesema, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekeza utekelezaji wa miradi ya maji yenye thamani ya Bilioni 45 kutatua changamoto ya Maji jijini Dodoma wakati ikisubiriwa utekelezaji wa Miradi ya kuleta maji kupitia Ziwa Victoria na mradi wa Bwawa la Farkwa.
Waziri Aweso ameyasema hayo leo wakati akishuhudia utiaji wa saini wa mkataba wa mradi wa kusambaza maji kupitia visima vya maji vya Nzuguni A wenye thamani ya Tsh 5bn unaotarajiwa kuwanufaisha watu 123,095.

“Mbunge wenu alileta maombi kwa Mh. Rais Samia juu ya uchimbwaji wa visima virefu wakati wa mkutano wa Mh. Rais pale Mpunguzi na sisi Wizara tukapata maelekezo ambayo tumeyafanyia kazi.

"Tunamshukuru Mheshimiwa Rais Samia kwa kulivalia njuga suala la maji hapa Jijini Dodoma kwa kuelekeza utekelezaji wa miradi ya maji ya zaidi Tsh 45bn ambayo itasaidia sana kupunguza tatizo la mgao wa maji katika maeneo mbalimbali."
DUWASA inaendelea na utekelezaji wa miradi mingine kama vile Nala (3.8bn), UDOM,(1.2bn), Mji wa Serikali (35.6bn), n.k.

Aidha wizara ya maji kwa kushirikiana na taasisi zake (DUWASA na RUWASA) imeunda timu zinazo endelea na Utafiti wa Maji chini ya Ardhi na Uchimbaji wa visima katika maeneo ya Mzakwe, Nzuguni, Kisasa, Nkuhungu, Miganga, Zuzu, Msalato na Ihumwa.
Naye Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde amesema utekelezaji wa mradi wa usambazaji kupitia Nzunguni utasaidia kupunguza adha ya mgao wa maji kwa wananchi wa maeneo ya Nkuhungu,Miganga,Chidachi,Nzuguni, Kisasa-Bwawani,Mwangaza, Ipagala, Ilazo, na Swaswa, Mpamaa na Njedengwa.
"Nipo hapa jijini Dodoma na kesho naanza ziara maalum kukagua utekelezaji wa miradi hii ili wananchi wa Dodoma wapate maji ya uhakika,"alisema Aweso.
Akitoa taarifa yake Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dodoma(DUWASA), Eng. Aron Joseph amesema Mradi huu unalenga kuhudumia watu wapatao 123,095.

Kukamilika kwa mradi huu kutapelekea ongezeko la uzalishaji kutoka lita milioni 81 hadi 91 kwa siku sawa na ongezeko la 30% kutoka chanzo cha Nzuguni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news