DODOMA-Benki Kuu ya Tanzania imeshiriki katika mkutano wa mwaka wa Chama cha Wanawake Katika Sekta ya Fedha (TAWIFA) uliofanyika tarehe 14 Aprili 2025, jijini Dodoma.
Mkutano huo uliwakutanisha wanawake kutoka taasisi mbalimbali ndani ya sekta ya fedha nchini, ukilenga kujadili masuala ya usawa wa kijinsia na ustawi wa wanawake katika maendeleo ya kiuchumi.

Mgeni rasmi katika mkutano huo alikuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko, ambaye aliipongeza TAWIFA kwa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake, huku akieleza mafanikio yaliyopatikana katika kipindi hicho kifupi.

Katika hotuba yake, Dkt. Biteko alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuwawezesha wanawake kwa kuondoa vikwazo vinavyowakabili na kuongeza fursa za kiuchumi na kijamii.


"Benki Kuu ya Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha usawa ndani ya sekta ya fedha. Tunaunga mkono jitihada za Mheshimiwa Rais katika kuhakikisha tunafikia usawa wa kijinsia kwa asilimia 50 kwa 50 ifikapo mwaka 2033," alisema Bi. Massawe.
Mkutano huu ni sehemu ya jitihada za kuimarisha mchango wa wanawake katika maendeleo ya kiuchumi, sambamba na kuendeleza majadiliano kuhusu masuala ya sera, uongozi, na fursa za kifedha kwa wanawake nchini.