Tanzania yaweka mikakati madhubuti katika Teknolojia ya Akili Unde (AI)

KIGALI-Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Tanzania, Mhe. Prof. Adolf Mkenda, amesema Tanzania imeongeza kasi katika kutumia na kuendeleza teknolojia ya Akili Unde (Ai) katika elimu kupitia utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali.
Ameyasema hayo Aprili 04, 2025, alipowasilisha mada kuhusu ajira na nguvu kazi katika eneo la Akili Unde (Ai) wakati wa mjadala wa wadau wa elimu na teknolojia duniani, uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kigali (KCC), Rwanda.
“Tanzania imeongeza kasi ya matumizi ya teknolojia za kidijitali ambayo ni dhamira ya Serikali ya Tanzania ya kuwawezesha vijana kupata mafunzo ya akili bandia na teknolojia zinazoibukia kupitia ufadhili wa masomo katika vyuo vikuu bora duniani.”

Prof. Mkenda amesema kuwa Serikali pia imeboresha Sera ya Taifa ya Elimu na Mafunzo pamoja na mitaala, kwa lengo la kuanza kuwajengea vijana uwezo wa TEHAMA ikiwemo Coding, kuanzia ngazi za chini za elimu

Mjadala huo pia ulihusisha washiriki mashuhuri wakiwemo Waziri wa Elimu wa Rwanda, Mhe. Joseph Nsengimana, Mkurugenzi wa Uchumi wa Kidijitali kutoka Mastercard Foundation, pamoja na wawakilishi kutoka China na sekta binafsi.
Kongamano hilo limekuwa jukwaa muhimu la kujadili mustakabali wa Afrika katika mapinduzi ya teknolojia ya Akili Unde (Ai), likilenga kuimarisha sera, elimu na uwekezaji unaolenga kizazi kijacho cha kidijitali.
Mjadala huo ni sehemu ya Kongamano la Akili Bandia barani Afrika, lililohitimishwa Aprili 04, 2025 na uliwaleta pamoja viongozi wa Serikali, wataalam wa teknolojia, na wadau kutoka sekta binafsi na mashirika ya kimataifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news