Wanadiplomasia wajionea maajabu ya Ngorongoro Crater

ARUSHA-Wanadiplomasia wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania, katika siku yao ya tatu za ziara yao wametembelea Bonde la Ngorongoro na kupata nafasi ya kuona mandhari nzuri ya bonde hilo lenye kuvutia na lenye wanyama aina tofauti wakiwemo wanyama watano wakubwa duniani.
Ziara hii pia imetoa fursa kwa Wanadiplomasia kuona rasilimali za kipekee za kiasili na za kitamaduni za Tanzania ambazo Wanadiplomasia hao licha ya kukaa nchini kwa muda mrefu, wengi wao hawakuwahi kuzitembelea na kuzifahamu kwa uhalisia wake.

Ziara hiyo ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje ambayo imejikita katika Diplomasia ya Uchumi imelenga kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania nje ya mipaka ya nchi.
Aidha, kupitia nafasi ya ushawishi waliyonayo Wanadiplomasia hao katika nchi zao, watasaidia kuwashawishi na kuhamasisha wananchi wa mataifa yao kutembelea nchini kwa wingi na kampuni za utalii za kimataifa kupata watalii wengi kuja Tanzania.

Vilevile, Wanadiplomasia wataendelea kujenga uhusiano binafsi na kubadilishana uzoefu katika kazi kutokana na umoja wanaoujenga katika ziara hii.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news