Rais Dkt.Mwinyi ashuhudia Fainali za Kombe la Shirikisho barani Afrika

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewaongoza maelfu ya mashabiki wa soka hapa nchini waliojitokeza kushuhudia Mchezo wa Fainali ya Michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika.
Mechi hiyo baina ya Simba SC na RS Berkane imechezwa katika Uwanja wa New Amaan Complex, ambapo kwa mara nyingine tena, Simba imeshindwa kutwaa kombe hilo baada ya kutoka sare ya bao 1–1.
Kwa matokeo hayo jumla ya magoli matatu kwa moja, RS Berkane kutoka Morocco imetawazwa kuwa Bingwa wa Kombe la Shirikisho kwa msimu wa 2024/2025.

Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amekabidhi kombe hilo kwa Nahodha wa RS Berkane, Issoufou Dayo.
Mechi hii ya fainali ya Michuano ya CAF ni ya kwanza kabisa kuchezwa Zanzibar, na hivyo kuandika historia mpya katika tasnia ya soka Barani Afrika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news