UDOM yawakabidhi bendera wanafunzi wa ICT kuelekea Fainali za Huawei

DODOMA-Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kupitia Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu (CIVE), kimewakabidhi rasmi bendera wanafunzi wanne wanaokwenda kuiwakilisha Tanzania katika Fainali ya Mashindano ya Kimataifa ya Huawei ICT Competition, yatakayofanyika nchini China.
Hafla hiyo, iliyofanyika Mei 16, 2025, iliongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Lughano Kusiluka, ambaye aliwapongeza wanafunzi hao Sigfrid Michael, Paul Nkingwa, Godlove Hipolite na Felix Kuluchumila na kuwahamasisha kurejea na ushindi.
Ndaki ya CIVE imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuipeperusha bendera ya UDOM kwenye mashindano mbalimbali ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) kwa ngazi ya kitaifa na kimataifa, ikiendelea kuthibitisha ubora wake katika nyanja hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news