Wafanyakazi wakoleza kasi ya ukuaji wa uchumi nchini

SINGIDA-Kasi nzuri ya ukuaji wa uchumi nchini, ambayo imefikia asilimia 5.5 kwa mwaka, imechangiwa kwa kiasi kikubwa na bidii, juhudi na kujituma kwa wafanyakazi katika sekta mbalimbali.
Ukuaji huu umeiwezesha Serikali kufanya maamuzi muhimu ya kuboresha ustawi wa wafanyakazi, ikiwemo kupandisha kima cha chini cha mishahara kwa watumishi wa umma kwa asilimia 35.1.

Hayo yalibainishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), yaliyofanyika kitaifa katika Viwanja vya Bombadia, mkoani Singida.
Wafanyakazi wa Benki Kuu ya Tanzania, wakiongozwa na Gavana Emmanuel Tutuba, walishiriki kikamilifu katika maadhimisho hayo, wakiungana na wenzao kutoka taasisi na mashirika mbalimbali kuadhimisha siku hii muhimu ya kutambua na kuenzi mchango wa wafanyakazi katika maendeleo ya Taifa.
Katika maadhimisho hayo, Bw. Melkiory E. Maria kutoka Kurugenzi ya Sarafu alitunukiwa Cheti pamoja na zawadi ya shilingi milioni 10 kwa kushinda nafasi ya kwanza katika Tuzo ya Mfanyakazi Bora wa Benki Kuu ya Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news