DCEA yatoa elimu kuhusu athari za dawa za kulevya kwa wanafunzi 3,000 wanaoshiriki UMISSETA

IRINGA-Wanamichezo zaidi ya 3,000 wanaoshiriki mashindano ya UMISSETA kitaifa mkoani Iringa wamepewa elimu kuhusu athari za dawa za kulevya.
Akizungumza wakati wa ufunguzi uliohudhuriwa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwijuma, Afisa Elimu Jamii Mwandamizi wa DCEA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Queen Komba amesema, elimu hiyo inalenga kuwakinga vijana dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya.
Ameongeza kuwa, matumizi ya dawa za kulevya huharibu afya ya akili, mwili, na nguvu kazi ya Taifa na Kutoa wito kwa vijana kuchukua hatua za makusudi kujiepusha na matumizi ya dawa hizo.
Mashindano ya UMISSETA mwaka huu yanajumuisha mikoa 28 na yanatarajiwa kufungwa Juni 29, 2025.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news