NILIPOAMKA asubuhi ile, nilikuwa na wasiwasi usio wa kawaida. Usiku mzima niliota nikiwa ndani ya chumba mahakamani nimesimama kizimbani nikijitetea mbele ya hakimu.
Nilikuwa navua viatu na kusujudu chini ya hofu, nikimuomba hakimu anisamehe kwa kosa ambalo hata kwenye ndoto sikuambiwa ni lipi. Niliamka nikiwa na jasho, moyo ukipiga kwa nguvu, lakini nikaipuuza kama ndoto za kawaida tu.
Lakini dakika chache baadaye, niliposikia hodi kali langoni na kufungua, nilijikuta nikiwa uso kwa uso na polisi wanne waliokuwa na hati ya kunikamata.

Walinitaja kwa jina langu kamili na kuniambia nina kesi ya udanganyifu wa kifedha ambayo imeripotiwa jana jioni na tayari mashitaka yamefunguliwa.
Nilipigwa na butwaa. Sikutegemea hata kidogo. Niliwauliza kosa hilo linahusu nini na lilitokea wapi, lakini hata wao walikuwa na taarifa finyu. Walinieleza tu kwamba nitajua zaidi...SOMA ZAIDI HAPA