Rais Dkt.Mwinyi aifariji familia ya marehemu Sheikh Jabir bin Haydar bin Jabir Al-Farsy

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi amejumuika na waumini wa Dini ya Kiislamu katika Sala ya Ijumaa iliyoswaliwa katika Masjid Mushawwar, Mwembe Shauri, Mkoa wa Mjini Magharibi leo Juni 6,2025.
Mara baada ya Sala ya Ijumaa, Rais Dkt. Mwinyi alifika nyumbani kwa familia ya marehemu Sheikh Jabir bin Haydar bin Jabir Al-Farsy eneo la Kikwajuni, Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi kutoa salamu za rambirambi pamoja na kuifariji familia hiyo kufuatia msiba wa Sheikh Jabir ulitokea tarehe 28 Mei 2025.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news