BoT yawaongezea maarifa wanafunzi mbalimbali Maonesho ya Sabasaba

DAR-Wanafunzi kutoka shule mbalimbali jijini Dar es Salaam wametembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere kuanzia tarehe 28 Juni hadi 14 Julai 2025.
Miongoni mwa shule zilizoshiriki ni Shule ya Msingi Gilman Rutihinda, Shule ya Sekondari Tusiime, na Shule ya Seminari ya Kisarawe. Wanafunzi kutoka shule hizo walipata fursa ya kujifunza kwa vitendo kuhusu majukumu na shughuli mbalimbali za Benki Kuu.
Pia, walielimishwa kuhusu alama za usalama zinazopatikana katika noti halali za Tanzania pamoja na njia sahihi za utunzaji wa noti hizo.
Kupitia ziara hiyo, wanafunzi wamehamasishwa kuwa mabalozi wa elimu ya fedha katika shule na jamii zao, wakichukua jukumu la kusambaza maarifa kuhusu masuala ya kifedha kwa lengo la kujenga jamii yenye uelewa mpana kuhusu uchumi na utunzaji bora wa noti.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news