Magazeti leo Julai 13,2025

MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imewataka wananchi wote wanaomiliki au kutumia ndege nyuki (drone) kuhakikisha wanazisajili ili kulinda usalama wa anga na kuzingatia sheria.
Akizungumza kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) Sabasaba, Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Salim Msangi, amesema usajili wa drone ni lazima na si hiari kwani zikitumika vibaya zinaweza kuhatarisha usalama wa taifa.

"Drone zinapaswa kusajiliwa kama ndege nyingine na zikitumika kiholela zinaweza kutumika kama silaha au kwa shughuli zisizo salama. Ndio maana tunasisitiza zisitumike bila kibali kutoka TCAA," amesema Msangi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news