Magazeti leo Julai 16,2025

DODOMA-Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza kuwa Kikao cha Kawaida cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kitafanyika Jumamosi, Julai 19, 2025 saa 4:00 asubuhi, katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM, jijini Dodoma.Kikao hicho kitaongozwa na Mwenyekiti wa CCM, na Rais Samia Suluhu Hassan.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (Itikadi, Uenezi na Mafunzo), CPA Amos Gabriel Makalla, amesema kwenye taarifa kuwa kikao hicho kinatanguliwa na vikao vya Sekretarieti ya CCM Taifa vinavyoendelea jijini Dodoma kwa ajili ya kupokea na kuchambua majina ya wagombea wa Ubunge na Baraza la Wawakilishi, majimbo na viti maalum.

Kikao cha Jumamosi kinatarajiwa kujadili ajenda mbalimbali muhimu, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.










Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news