Magazeti leo Julai 20,2025

MKUU wa Mkoa wa Kigoma, Kamishna wa Polisi mstaafu, Simon Sirro amesema pato la Mkoa limeongezeka kutoka Sh trilioni 4.1 mwaka 2020 hadi Sh trilioni 5.6 mwaka 2024, sawa na ukuaji wa asilimia 38.6, ikiwa ni matokeo ya jitihada za serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan.
Aidha, pato la mwananchi Kigoma limepanda kutoka milioni 1.4 hadi milioni 2.1 katika kipindi hicho, sawa na ongezeko la asilimia 45.4.
Ameyasema hayo Julai 19,2025 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea mafanikio ya miaka minne ya serikali ya awamu ya sita

Sirro amesema, Kigoma ina fursa nyingi za uwekezaji kutokana na jiografia ya kipekee, ardhi yenye rutuba, vivutio vya utalii na uwepo wa Ziwa Tanganyika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news