Stephanie Aziz Ki kurejea Yanga SC

DAR-Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Yanga SC,Ally Kamwe amesema,Stephanie Aziz Ki anatarajiwa kurejea klabuni hapo.

Ni kutokea klabu ya Wydad Casablanca baada ya kumaliza mkataba,kwani makubaliano yao ilikuwa ni kuwatumikia Wydad kwa mkataba wa miezi mitatu.
Amesema kwamba, mkataba huo una vipengele viwili ambapo ikiwa klabu hiyo ya Morocco itaridhishwa na kiwango chake basi watamuongezea mkataba wa miaka miwili na ikiwa vinginevyo basi atarejea Yanga SC na atakuwepo kwenye mchezo wa Ngao ya Jami.

Kamwe ameeleza kuwa,kwa mujibu wa makubaliano ilikuwa hadi kufikia Julai 10,mwaka huu Wydad wawe wameshawasiliana na Yanga SC.

"Kama Wydad watakuwa wanaongeza maana yake wamalizie kiasi ambacho tulikubaliana ila kama watasema arudi sawa arudi aje awashone maana bado amebaki na mwaka mmoja."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news