Magazeti leo Februari 17,2026

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) inashiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo yanayofanyika nchini Qatar ikiwa ni sehemu ya mkakati wake wa kupanua wigo wa ushirikiano wa kimataifa, kuvutia uwekezaji na kuimarisha sekta ya kilimo nchini.
Ushiriki huu unaonesha dhamira ya TADB katika kuifanya sekta ya kilimo kuwa ya kisasa, yenye tija. Ushiriki katika jukwaa la kimataifa kama hili unatoa nafasi ya kubadilishana uzoefu, teknolojia na mbinu bora za kilimo kutoka mataifa mbalimbali.

Maonesho ya kimataifa ya kilimo Qatar yanawakutanisha wadau kutoka nchi tofauti wakiwemo wawekezaji, taasisi za kifedha za kimaendeleo, wataalamu wa teknolojia za kilimo, wasambazaji wa pembejeo, na watunga sera.

Kwa TADB, hii ni fursa adhimu ya kujenga mitandao kimkakati itakayosaidia kuongeza upatikanaji wa rasilimali fedha na utaalamu kwa ajili ya kukuza kilimo Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here