Waajiri kutoka Sekta Binafsi wametakiwa kuwapa nafasi na kuwazingatia vibarua wanaposajili wafanyakazi kwenye mfumo ili kuweza kutambulika kwenye mfumo na kuleta tija, usawa katika maeneo ya kazi.
Ameyasema hayo, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi Ajira na Mahusiano Godwin Mpelumbe wakati akitoa Mafunzo ya Mfumo wa Taifa wa Kielektroniki wa Taarifa za Soko la Ajira kwa Waajiri hao Februari 24, 2026 katika Ukumbi wa NSSF jijini Dar es salaam.Aidha, mafunzo hayo yalilenga kuwapatia uwezo katika utoaji taarifa za ajira wakiwa maeneo ya kazi ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo






























