DODOMA-Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), amewasisitiza watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi, uadilifu na kufuata sheria, Kanuni na miongozo ya utumishi wa umma.
Amesema, hatua hiyo itaendelea kukuza weledi katika kazi kwa watumishi wa wizara, na hivyo kujenga na kuimarisha taswira ya wizara ndani na nje ya nchi.
Amesema, hatua hiyo itaendelea kukuza weledi katika kazi kwa watumishi wa wizara, na hivyo kujenga na kuimarisha taswira ya wizara ndani na nje ya nchi.Waziri Kombo ametoa rai hiyo alipokutana na watumishi wa wizara katika kikao kazi kilichofanyika jijini Dodoma.
“Leo tumekutana wote kwa mara ya kwanza, watumishi wenzangu hamna budi kufanya kazi kwa ufanisi na mzingatie maadili na kufuata sheria, kanuni na miongozo ya utumishi wa umma ili kujenga na kuimarisha taswira ya wizara yetu ndani na nje ya nchi na kulinda maslahi mapana ya nchi,” alisema Mhe. Waziri.
Amebainisha kuwa, watumishi wana dhamana kubwa ya kusimamia na kutekeleza diplomasia ya uchumi, jambo linalohitaji uzalendo katika kutekeleza majukumu ya kila siku ya wizara.

Mhe. Kombo amesema ni muhimu watumishi kuondokana na dhana ya kufanya kazi kwa mazoea kwani nyakati hizi haziendani na dhana hiyo, huku akisisitiza Watumishi
katika sehemu ya kazi kujiendeleza kitaaluma na ili kumudu kasi ya mabadiliko na hivyo kuiwezesha Wizara kufikia malengo ambayo imejiwekea.
“Hizi ni zama za AI-Akili mnemba, kila mmoja anapaswa kujituma , kujiongeza na kujiendeleza ili kuendana na mahitaji ya wakati huu tuliopo na hivyo kufikia malengo ya kimkakati ambayo wizara imejiwekea,” alisisitiza Mhe. Waziri.
Katika kikao hicho, Mhe.Waziri Kombo amewapongeza Watumishi wa Wizara kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya na kuwasihi kuendelea na moyo huo.













