Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimesisitiza umuhimu wa kuwekeza katika tafiti, ubunifu na teknolojia za uzalishaji wa mbegu bora ili kuongeza tija katika sekta ya kilimo na kuimarisha usalama wa chakula nchini.
Kauli hiyo imetolewa wakati wa mjadala wa masuala ya uwekezaji katika miradi ya maendeleo ya uzalishaji wa mbegu na ubunifu wa teknolojia za kilimo ulioandaliwa na SUA kwa kushirikisha wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo, wakiwemo watafiti, taasisi za kifedha, wazalishaji wa mbegu na Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI).
Akizungumza kwa niaba ya Makamu Mkuu wa SUA, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalam, Prof. Maulid Mwatawala, alisema maendeleo ya sekta ya kilimo yanategemea kwa kiwango kikubwa uwekezaji katika teknolojia rahisi, tafiti na ubunifu unaolenga kutatua changamoto zinazowakabili wakulima.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo




























