Idadi ya vifo 518 imepatikana kwenye vyanzo rasmi kama Wizara ya Afya na wafiwa wenyewe-Balozi Msuya

DAR-Mjumbe wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Oktoba 29, Balozi Radhia Msuya ametoa ufafanuzi kuhusu idadi ya vifo iliyobainishwa katika ripoti ya tume hiyo.
Amesema, idadi hiyo imezingatia taarifa kutoka kwenye vyanzo rasmi kama vile Wizara ya Afya pamoja na ushahidi uliotolewa na mashuhuda waliojitokeza mbele ya tume wakati wa uchunguzi.

Balozi Msuya ameeleza kuwa,takwimu hizo zinawakilisha hali halisi hadi wakati tume inakamilisha uchunguzi wake, na kwamba zinaweza kubadilika endapo kutapatikana taarifa nyingine mpya na sahihi kutoka kwa mamlaka husika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here