Rais Ruto awasili Dodoma,kuhutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

DODOMA-Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. William Samoei Ruto amewasili jijini Dodoma Mei 5, 2026 kuendelea na ziara yake ya kitaifa ya siku mbili hapa nchini.
Mhe. Rais William Ruto mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo na Viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Rosemary Senyamule.
Akiwa Dodoma, Mhe. Rais William Ruto atahutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni mara ya kwanza kwa Rais huyo kuhutubia Bunge hilo na ikiwa ni mara ya pili kutembelea Dodoma baada ya ziara yake ya mwaka 2022.

Aidha, baada ya shughuli hiyo Bungeni, Mhe. Rais William Ruto ataelekea Ikulu ya Rais iliyopo Chamwino ambapo atapokelewa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Akiwa Ikulu, Chamwino, pamoja na mambo mengine Mhe. Rais William Ruto ataagana na mwenyeji wake, Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Viongozi wa Serikali ya Tanzania kabla ya kuondoka nchini kutokea Dodoma kurejea nchini kwake.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here