NA DIRAMAKINI
SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) limetangaza kusimama kwa huduma za treni za Reli ya Kisasa (SGR) kutokana na hitilafu iliyotokea katika mfumo wa Gridi ya Umeme ya Taifa.
Kupitia taarifa iliyotolewa leo Juni 27, 2026 na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa TRC, Fredy Mwanjala ni kwamba shirika hilo limewaomba radhi abiria wote walioathirika na usumbufu uliojitokeza kutokana na kusimama kwa huduma hizo.
TRC imesema wataalamu wake kwa kushirikiana na wataalamu wa TANESCO wanaendelea kufanya kazi kwa pamoja ili kurejesha huduma za treni haraka iwezekanavyo.
Shirika hilo limewahakikishia Wananchi kuwa jitihada zinaendelea kuhakikisha huduma zinarejea katika hali ya kawaida mara tu hitilafu hiyo itakapopatiwa ufumbuzi.
