DODOMA-Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa anawatangazia waombaji wote wa ajira waliofanya mtihani wa kuandika kutembelea akaunti zao za maombi ya ajira kupitia mfumo wa ajira wa TAKUKURU "https://ajira.pccb.go.tz" na kwa barua pepe zao ili kupokea taarifa na maelekezo ya tarehe, muda na eneo la kufanyia usaili wa ana kwa ana (Oral Interview) kwa waliofaulu
Mambo muhimu ya kuzingatia: -
1. Kila aliyeitwa kwenye usaili anatakiwa kufika kwa siku na muda aliopangiwa akiwa na nyaraka zifuatazo: -
1.1. Nakala halisi za vyeti vya masomo (Taaluma na kozi mbalimbali)
1.2. Picha tatu "Passport Size"
1.3. Nakala halisi ya cheti cha kuzaliwa
1.4. Kitambulisho cha taifa (NIDA)
1.5. Majina ya wadhamini wawili, anwani zao na namba za simu.
2. Kuwasilisha nyaraka za kugushi ni kosa la Jinai
3. Kila atakayefika kwenye usaili huu anapaswa kujigharamia
Imetolewa na
Mkurugenzi Mkuu,
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa,
1 Mtaa wa TAKUKURU,
S.L.P. 129,
41101 DODOMA.
