Ndege ya abiria ya Jeshi aina ya Antonov An-26 (turboprop) ambayo ilikuwa imebeba watu 28 inaripotiwa kuanguka mjini Kharkov Kaskazini Mashariki mwa Ukraine na kuua watu 22.
(Idara ya Dharura/AP). |
Ajali hiyo ilitokea majira ya leo saa 20:50 kwa saa za huko (19:50 CET) karibu na mji wa Mashariki wa Chuhuyiv, katika Mkoa wa Kharkiv, umbali wa kilomita mbili kutoka uwanja wa ndege wa kijeshi.
Watu 28 waliokuwemo ndani ya ndege ya AN-26 walikuwa marubani wa kijeshi na maafisa wa Chuo Kikuu cha Kikosi cha Anga cha Kozhedub. Awali wizara ilikuwa imesema kuwa watu 24 walikuwa kwenye ndege wakati ikianguka.