Sudan imekubali kuilipa Marekani dola milioni 335 kama fidia ya vitendo vya ugaidi

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema kuwa, Serikali mpya ya Sudan imekubali kuilipa Marekani dola milioni 335 kwa ajili ya waathirika na familia zilizoguswa na vitendo vya kigaidi,anaripoti Mwandishi Diramakini.

Ameyasema hayo leo Oktoba 19,2020 kupitia taarifa iliyoonwa na Mwandishi Diramakini katika ukuta wake wa Facebook.

"Habari njema,Serikali mpya ya Sudan iliyopo katika mchakato imekubali kulipa dola milioni 335 kwa Marekani kwa ajili ya waathirika na familia zilizoguswa na ugaidi.

"Pindi watakapofanya malipo hayo, nitaiondoa Sudan katika orodha ya wafadhili wa magaidi, hii ni hatua kubwa kwa ajili ya haki ya Wamarekani na hatua muhimu kwa Sudan,"ameeleza.



Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news