Tetesi:Manchester United inaweza kuingia kandarasi na Jadon Sancho,Luis Gomes

Kwa mujibu wa Mail, Kocha wa West Ham, David Moyes amesema alikuwa na helikopta tayari kumchukua juu kwa juu juu, Gareth Bale (31), mshambuliaji wa Wales ambaye karibuni alirejea Spurs, ambaye alitoka Tottenham na kuelekea Real Madrid mwaka 2013 wakati huo akiwa kocha wa Manchester United.

Huku Sun ikiripoti kuwa, winga wa Wolves, Adama Traore (24) yuko tayari kupokea wito wa Barcelona na Liverpool ili kusaini kandarasi mpya ya pauni 100,000 kwa wiki huko Molineux, mshambuliaji huyo wa Hispania alijiunga na klabu hiyo akitokea Middlesbrough mwaka juzi.
Winga wa Borussia Dortmund na England, Jadon Sancho. (Football Empire).

Pia Manchester United imepewa matumaini kwamba, inaweza kusaini mkataba na winga wa Borussia Dortmund na England, Jadon Sancho (20), hiyo ikiwa ni kwa mujibu wa Star huku Mirror ikiripoti kuwa, klabu hiyo pia imemlenga kiungo wa kati wa Sporting Lisbon, Luis Gomes (16).

Kwa mujibu wa Daily Telegraph, mchezaji na kocha wa Derby County, Wayne Rooney (34) anatarajia kupata matokeo ya vipimo vya Corona leo ikiwa ni baada ya kugundua kuwa rafiki yake aliyemuuzia saa ya mkononi alikuwa na COVID-19.

Wakati huo huo, Mail inaripoti kuwa, mlinzi wa zamani wa Liverpool, Jamie Carragher anasema klabu hiyo lazima imsaini kiungo wa safu ya kati baada ya Virgil van Dijk (29) kupata majeraha wakati wa mechi yao dhidi ya Everton hivi karibuni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news