Balozi Kairuki atoa wito maalum kwa China kuhusu Afrika

Mjadala wa Mabalozi, Wanazuoni na wafanyabiashara umefanyika leo jijini Beijing,China kuzungumzia Mpango wa 14 wa Maendeleo wa China na fursa za ushirikiano na mataifa ya Nje, anaripoti Mwandishi Maalum Diramakini (Beijing).

Katika mkutano huo ambao pia Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki ameshiriki wamejadili pia fursa za uchumi katika Eneo la Soko Huru la Afrika (AfCFTA).

Katika mkutano huo Balozi Kairuki ametoa wito kwa China na Afrika kushirikiana kuongeza tija katika sekta ya kilimo kuongeza uzalishaji wa malighafi za kutosheleza mahitaji ya soko la ndani na nje.
Pia Balozi Kairuki amehimiza uwekezaji katika kuongeza thamani ya malighafi ili kuweza kuzalisha bidhaa zitakazouzwa Barani Afrika na nje ya nchi. Bila kufanya hivyo, mpango wa Soko Huru la Afrika hautakuwa na manufaa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news