Mkuchika aipa kongole TPSC ujenzi jengo litakaloboresha utoaji mafunzo

Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kimepongezwa kwa kutumia fedha za mapato yake ya ndani kiasi cha shilingi bilioni 3.5 kujenga jengo la ghorofa mbili lililoanza kutumika kutoa mafunzo kwa watumishi wa umma na wananchi katika fani mbalimbali zinazotolewa na chuo hicho kwenye Kampasi ya Tabora, anaripoti James K.Mwanamyoto (OR-Utumishi).
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt. (Mst) Mhe. George Mkuchika akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) - Kampasi ya Tabora (hawapo pichani) alipoenda kukagua jengo jipya la TPSC Kampasi ya Tabora. (Picha na OR-Utumishi).

Pongezi hizo zimetolewa mkoani Tabora na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (Mst), George Mkuchika mara baada ya kukagua jengo jipya la TPSC Kampasi ya Tabora.

Waziri Mkuchika amesema, hatua ya kutumia fedha za ndani kujenga jengo lenye ofisi na madarasa, linapaswa kuigwa na taasisi nyingine za umma ambazo zinaitegemea Serikali kuwapatia fedha kuboresha ofisi zao.
Muonekano wa jengo jipya la Chuo Cha Utumishi wa Tanzania (TPSC) - Kampasi ya Tabora lililojengwa kwa fedha za mapato ya ndani.(OR-Utumishi).
Baadhi ya wanafunzi wakipata mafunzo katika moja ya darasa lililopo ndani ya jengo jipya la Chuo Cha Utumishi wa Tanzania (TPSC) -Kampasi ya Tabora lililojengwa kwa fedha za mapato ya ndani. (OR-Utumishi).

“Kitendo cha kutumia fedha za ndani kwa maendeleo ya taifa ni jambo zuri ambalo Mheshimiwa Rais amekuwa akisisitiza mara kwa mara, hivyo, ujenzi wa jengo hili linanipa ujasiri wa kuwaalika wiongozi wa Kitaifa kulizindua rasmi, huku kipaumbele kikiwa kwa Mheshimiwa Rais mwenyewe,”amefafanua Mkuchika.

Pia Waziri Mkuchika ameongeza kuwa, ushirikiano na uadilifu uliopo baina ya viongozi na watumishi ndio ulifanikisha kukamilika kwa ujenzi wa jengo hilo, hivyo amewataka kuuendelea na utamaduni huo kwa masilahi ya chuo na maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt. (Mst) Mhe. George Mkuchika akishuhudia mpangilio wa vitabu katika maktaba maalum iliyoko kwenye jengo jipya la Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) - Kampasi ya Tabora. (Picha na OR-Utumishi).
Baadhi ya watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzani-Kampasi ya Tabora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt. (Mst) Mhe. George Mkuchika (hayupo pichani) alipoenda kukagua jengo jipya la TPSC Kampasi ya Tabora. (OR-Utumishi).
Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Emmanuel Shindika akiwasilisha kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt. (Mst) Mhe. George Mkuchika taarifa ya mradi wa jengo jipya la TPSC-Kampasi ya Tabora alipoenda kukagua jingo hilo. (OR-Utumishi).

Akitoa taarifa kuhusu ujenzi wa jengo hilo, Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Emmanuel Shindika amesema, jengo hilo limekamilika na kuanza kutumika kabla ya uzinduzi rasmi ili kuongeza ufanisi kiutendaji na kubaini mapungufu yanayoweza kujitokeza kwa lengo la kuyadhibiti.

Mradi wa ujenzi wa jengo hilo linalojumuisha maktaba, vyumba vya madarasa ya kompyuta, kumbi, madarasa ya kawaida na ofisi za watumishi ulianza Novemba 5, 2014 na kukamilika rasmi Machi 26, 2020. 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt. (Mst) Mhe. George Mkuchika akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania-Kampasi ya Tabora alipoenda kukagua jengo jipya la TPSC Kampasi ya Tabora. (OR-Utumishi).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news