Matumizi ya Tiketi Mtandao kwenye mabasi kuanza kesho nchini

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Ardhini (LATRA) imetangaza kuanza kwa matumizi ya Tiketi za Kieletroniki kwenye Mabasi yanayokwenda Mikoani na kwa watakaoshindwa kufanya hivyo wasitishe kutoa huduma kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria, anaripoti Mwandishi Diramakini.
Maamuzi haya yanasimamiwa na Kanuni ya 4(2)(c); Leseni ya kusafirisha abiria itatolewa kwa muombaji aliyesajiliwa kwenye mfumo wa tiketi za kielektroniki ulioidhinishwa na Mamlaka.

Pia, Kanuni ya 24(b)(d); Msafirishaji mwenye leseni ya kusafirisha abiria wa masafa marefu ahakikishe anatoa tiketi za kielektroniki kwa abiria.

LATRA imesema, kupitia mfumo huu, Wananchi watatumia simu kukata tiketi jambo litakaloepusha wizi, ulanguzi wa tiketi na adha za wapiga debe. Pia, unalenga kukomesha vitendo vya upandishaji holela wa nauli hasa kipindi cha mwisho wa mwaka.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news