Rais Magufuli ampokea Rais Nyusi mjini Chato

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshuhudia mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akimwagilia maji mti alioupanda baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita alikowasili kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Janruari 11, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi katika Ikulu ndogo ya Chato mkoani Geita baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Janruari 11, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi zawadi ya picha ya kuchora ya THE BIG FIVE mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi katika Ikulu ndogo ya Chato mkoani Geita baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Janruari 11, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakimsikiliza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita alikowasili kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Janruari 11, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakisikiliza maelezo toka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto kabla ya kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita leo Jumatatu Janruari 11, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulisha kwa viongozi mbalimbali mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi aliopowasili ili kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita leo Jumatatu Janruari 11, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakifurahia ngoma za utamaduni katika Uwanja wa Ndege wa Geita mara alipowasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Janruari 11, 2021. (Picha zote na Ikulu).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news