Ripoti ya kuungua Soko Kuu Kariakoo yatua kwa Waziri Mkuu

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo, Julai 27, 2021 amepokea taarifa ya Kamati ya Uchunguzi wa tukio la moto uliotokea katika soko la kimataifa la Kariakoo tarehe 10 Julai, 2021 jijini Dar es salaam.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea taarifa ya Kamati ya Uchunguzi wa tukio la moto uliounguza Soko Kuu la Kariakoo kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo CP Liberatus Sabas kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam, Julai 27, 2021. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Uchunguzi wa tokio la moto uliounguza Soko Kuu la Kariakoo baada ya kupokea taarifa ya Kamati hiyo kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam, Julai 27, 2021. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Uchunguzi wa tukio la moto uliounguza soko la Kariakoo baada ya kupokea taarifa ya Kamati hiyo kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam, Julai 27, 2021. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Mheshimiwa Majaliwa amepokea taarifa hiyo kutoka kwa mwenyekiti wa Kamati hayo, CP Liberatus Sabas na kuahidi kuwa serikali itayafanyia kazi mapendekezo yote yaliyotolkewa na Kamati hiyo.

Akizungumza baada ya kuipokea taarifa hiyo kwenye Makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam, Mheshimiwa Majaliwa amewashukuru na amewapongeza wajumbe wa Tume hiyo kwa kazi nzuri iliyofanyika kwa weledi mkubwa.

Mheshimiwa Majaliwa amesema ataifikisha taarifa hiyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwani tukio hilo limewagusa watu ndani na nje ya nchi.

“Naahidi mbele yako Mwenyekiti kuwa Serikali imeridhishwa na taarifa mlioyo nikabidhi leo na mapendekeso yote mliyoyatoa yatazingatiwa,"amesema.


Jumapili Julai 11, 2021 Mheshimiwa Majaliwa alipotembelea na kukagua hatua zinazoendela kuchukuliwa kudhibiti moto katika soko la kimataifa la Kariakoo alitangaza kamati ambayo ilipewa kazi ya kuchunguza tukio hilo ili kubaini chanzo cha moto huo.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo CP Liberati Sabas amezishukuru Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na wajumbe wengine katika timu hiyo kwa ushirikiano walioutoa katika kufanikisha kazi hiyo "Mheshimiwa Waziri Mkuu kama haya tuliyoyabaini yakifanyiwa kazi matukio kama hayo hayatajirudia"


Kamati hiyo aliyoundwa ambayo ilifanya kazi na kamati ya ulinzi na usalama iliyoanza kufanya kazi chini ya Mkuu wa Mkoa huo ilijumuisha Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu (Idara ya Maafa).


Wengine ni Vyombo vya Ulinzi na Usalama ikujumuisha Jeshi la Wananchi, Jeshi la Polisi, Zimamoto, Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU). Pia Waziri Mkuu alizitaja Wakala wa Majengo, Shirika la Umeme (TANESCO), Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na Ofisi ya Taifa ya mashtaka, Wakala wa Umeme na Ufundi Tanzania (TEMESA)

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news