Katibu wa Ofisi ya Mbunge wa Kibaha Vijijini ajiuzulu

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Katibu wa Ofisi ya Mbunge wa Kibaha Vijijini, Johari Marijani ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo.
Johari ameyasema hayo kupitia taarifa kwa umma aliyoitoa leo Agosti 20,2021.a

"Naomba kuufahamisha umma wa Kibaha Vijijini kwamba kuanzia sasa, mimi JOHARI MARIJANI si Katibu tena wa Ofisi ya Mbunge wa Kibaha Vijijini. Nimejiuzulu."Sababu ya kujiuzulu ni kuelemewa na majukumu ya Ofisi ya Mbunge na majukumu mengine mengi yanayonihusu, huku majukumu ya pande zote yakiwa na umuhimu mkubwa na uzito unaokaribiana. Kwa hiyo, nimechagua kutokuwa mkwamishaji wa majukumu muhimu ya Ofisi ya Mbunge kwa kuamua kujiuzulu.

Namshukuru sana Mhe Mbunge kwa imani na ushirikiano mkubwa alionipatia kwa kipindi chote ambacho nimefanya naye kazi.

"Aidha, nawashukuru pia wananchi na wadau wote wa Jimbo la Kibaha Vijijini kwa kushirikiana nami vema kwa kipindi chote ambacho nimehudumu katika Ofisi hii. Namtakia kila la kheri Mhe Mbunge anapojipanga upya kuendeleza vema huduma za Ofisi hii bila uwepo wangu,"amefafanua aliyekuwa Katibu wa Ofisi ya Mbunge wa Kibaha Vijijini aliyejiuzulu,Johari Marijani.

Jimbo la Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani linaongozwa na Mheshimiwa, Michael Mwakamo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news