BREAKING NEWS: Tanzania kupokea ndege zake mpya aina ya Airbus A220-300

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Ndege mpya mbili aina ya Airbus A220-300, zilizonunuliwa na Serikali ya Tanzania zimeondoka nchini Canada kuja Tanzania.
Kwa mujibu wa Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ndege hizo zitapokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sheikh Abeid Amani Karume Mjini Unguja, Zanzibar kesho Oktoba 8, 2021 majira ya saa 9:00 Alasiri na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.
Ndege hizi zitakamilisha hesabu ya ndege 11 zilizonunuliwa na kuwasili hapa nchini.

Ndege nyingine 5 (Boeing 787-8 Dreamliner (2), Airbus A220-300 (2) na Bombardier Dash 8 Q400 (1) zimeshalipiwa na zitakuja baadaye.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news