Balozi Meja Jenerali mstaafu Issa Suleiman Nassor atembelea vyanzo vya maji vya ZAWA Kusini Unguja

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA), Balozi Meja Jenerali mstaafu Issa Suleiman Nassor leo ameendelea na ziara yake siku ya pili kwa kutembelea maeneo ya vyanzo vya maji vya ZAWA Mkoa wa Kusini Unguja.
Balozi Meja Jenerali Mstaafu Issa Suleiman Nassor, ametembelea chanzo cha maji safi na salama ya Machomwe Kizimkazi, kinachozalisha maji na kusambaza katika kijiji hicho.

Aidha, ametembelea visima vya maji vya Makunduchi, Jambiani Mfumbwi, Kijuuni na Kivulini.

Pia, ametembelea kisima cha maji cha Bwejuu – Michamvi na Ukongoroni.
Akifanya majumuisho baada ya ziara hiyo, Balozi Meja Jenerali Mstaafu Issa Suleiman Nassor amesema,watendaji wa ZAWA wanatakiwa kuboresha huduma ya maji safi na salama pamoja na kushirikiana vyema na taasisi nyingine ili kutatua baadhi ya changamoto zilizopo katika maeneo hayo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news