Wanawake wang'ara mchakato wa kumrithi Ndugai nafasi ya Uspika, ADC yamtangaza Maimuna Said Kassim

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

CHAMA cha Alliance for Democratic Change (ADC) kimemtangaza, Maimuna Said Kassim kuwa mgombea wa nafasi ya uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Maimuna ametangazwa kwenda kuwania nafasi hiyo ambayo iliachwa wazi hivi karibuni na Spika wa Bunge hilo, Mheshimiwa Job Ndugai baada ya kujiuzulu.

Baada ya kutangazwa kuteuliwa na chama hicho leo Januari 21, 2022 jijini Dar es Salaam, Maimuna amekishukuru chama chake kwa kumuamini na kumpatia fursa ya kwenda kupambana kwenye nafasi hiyo ambayo pia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemteua Mheshimiwa Dkt.Tulia Ackson.

"Kikubwa nitahakikisha Bunge letu linakuwa la kisasa na linaenda kutenda haki kuhakikisha linasimamia maslahi ya Watanzania,” amesema Maimuna. 

Pia amesema, uwezo katika nafasi ya ungozi ni moja ya mambo yaliyomsukuma kuwania nafasi hiyo huku akielezea endapo atapata nafasi atahakikisha miimili yote ya Serikali kwa maana ya Serikali, Bunge na Mahakam inafanya kazi kwa ushirikiano.

Kwa upande wake,Mwenyekiti wa chama hicho, Hamad Rashid ameeleza kuwa Maimuna anatosha kushika nafasi hiyo baada ya kupikwa ndani ya chama hicho.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news