Waziri Mkenda atoa maelekezo kwa TARI kuhusu mbolea inayozalishwa nchini

NA MATHIAS CANAL-WK

WAZIRI wa Kilimo, Profesa Adolf Mkenda ameiagiza Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kutengeneza vipeperushi ambavyo vitasambazwa kwenye halmashauri za wilaya nchini ili kuitangaza mbolea ya hapa nchini.
Waziri wa Kilimo, Profesa Adolf Mkenda akikagua maghala ya kuhifadhia mbolea ya Minjingu wakati alipofanya ziara ya kikazi katika kiwanda cha mbolea cha Minjingu Wilaya ya Babati mkoani Manyara, Januari 7,2022. 
Waziri wa Kilimo, Profesa Adolf Mkenda akisisitiza jambo wakati alipofanya ziara ya kikazi katika kiwanda cha mbolea cha Minjingu Wilaya ya Babati mkoani Manyara.

Kauli hiyo ameitoa Januari 7, 2022 wakati alipofanya ziara katika kiwanda cha Minjingu kilichopo Wilaya ya Babati Mkoa wa Manyara akiongozana na Mkurugenzi wa Mazao Wizara ya Kilimo, Nyasebwa Chimagu, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Stephan Ngailo, Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo (TARI-Mlingano), Dkt.Catherine Senkoro.
Waziri wa Kilimo, Profesa Adolf Mkenda akisisitiza jambo wakati alipofanya ziara ya kikazi katika kiwanda cha mbolea cha Minjingu Wilaya ya Babati mkoani Manyara. 

Profesa Mkenda amesema, kwa sasa wanataka kufanya tathimini kama mbolea iuzwe nje kwa kiasi gani hususani ambayo haitumiki hapa nchini bila hivyo mantiki ya kiuchumi haina maana yoyote.

"Vipeperushi vitengenezwe na TARI mshirikiane na wenzenu muandike maneno tupeleke mkoani haraka watu wajue ipi ya kuoteshea mazao gani na ndani ya wiki mbili tuwe tumehamasisha halafu tuangalie mbolea inakwenda kiasi gani tukiona kwamba bado ipo ya kutosha tutafanya tathimini haraka kwamba bado tuendelee kuzuia na tunazuia ili nini," amesema Prof Mkenda.

Aidha, amemtaka Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mazao kushirikiana na maafisa ugani kuwekeza maeneo yanayozalisha chakula kwa wingi ili kuondokana na hali ya utegemezi pindi kunapotokea changamoto ya chakula.
Sehemu ya washiriki wa kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa kiwanda cha mbolea ya Minjingu wakifuatilia kwa karibu maelekezo ya Waziri wa Kilimo, Profesa Adolf Mkenda wakati alipofanya ziara ya kikazi katika kiwanda cha mbolea cha Minjingu Wilaya ya Babati mkoani.

"Tutafute maeneo ya kufanya mbolea hii kama shamba darasa, tutangazie maafisa ugani Kwa kushirikiana na TARI na TFRA tutumie vipeperushi vya wizara kuitangaza mbolea ya ndani ya nchi ili kiwanda cha mbolea kifanye kazi vizuri,"amesisitiza Waziri Mkenda.

"Kiwanda kama hiki kisiposimama mkakati wetu hautaenda vizuri, kiwanda Cha mbolea kilichopo Dodoma tayari niliagiza Mkurugenzi wa Maendeleo ya mazao tumempeleka nchini Burundi kwenda kujifunza ndio amerudi nasubiri taarifa.

"Nenda huko kaangalie mbolea kama tunaweza kununua kidogo, lakini tuchukue uzoefu ambao tunaweza kutumia ili kama kile kiwanda kikifunguliwa tuwe na kauli ya kusema na sisi tumejaribu mahali fulani tumeona efficiency yake, sasa hatuwezi kufanya hivyo kwa kiwanda ambacho hakifanyi kazi,"amesema.

Aliwahakikishia kuwa atazungumza na Katibu Mkuu ili kutafuta bajeti za kutengeneza vipeperushi ili kusambaza kwenye kila wilaya ili kuhakikisha vinawafikia watu wengi zaidi.
Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha Mbolea ya Minjingu, Tosk Hans akizungumza mbele ya Waziri wa Kilimo, Profesa Adolf Mkenda wakati alipofanya ziara ya kikazi katika kiwanda cha mbolea cha Minjingu Wilaya ya Babati Mkoani Manyara. (Picha zote na Mathias Canal-WK).

Awali, Mkurugenzi wa Kiwanda cha Minjingu kilichopo Wilaya ya Babati mkoani Manyara, Tosk Hans alisema wametii agizo la kupeleka mbolea ya kutosha mikoa ya Kanda ya kusini huku mikoa ya Iringa, Mbeya, Njombe, Songea, Rukwa, Sumbawanga yote ina mbolea ya kutosha ya kupandia na kulimia licha ya kuwa na changamoto ya mvua.

"Bei yetu ni rafiki hatutakuangusha kwani mkoa wa mbeya tumepeleka Tani 6200, mpaka mwisho wa msimu, tuna tani 1600 ambazo zipo mikoa ya kusini, huku tu angoja hadi msimu utakapoanza, ipo ya kutosha na bado ikihitajika tutapeleka na tuna tani 9000 zipo kwenye maghala hapa kiwandani ikingoja kwenda mahali popote itakapotokea changamoto ya mbolea," amesema Hans.

Ameongeza kuwa, hawakusafirisha mbolea nje ya nchi mpaka changamoto ya ndani iishe, hivyo kuomba mchakato huo uanze kama wataruhusiwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news