Viwango elekezi vya kubadilisha fedha za kigeni leo Februari 10, 2022

GODFREY NNKO

LEO Yuan ya China inanunuliwa kwa shilingi 359.4 huku ikiuzwa kwa shilingi 362.9 na Yen ya Japan inanunuliwa kwa shilingi 19.8 na kuuzwa kwa shilingi 20.005.

Franka ya Burundi inanunuliwa kwa shilingi 2.19 na kuuzwa kwa shilingi 2.206 huku dola ya Marekani nchini ikinunuliwa kwa Shilingi 2286.67 huku ikiuzwa kwa Shilingi 2309.56.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya viwango elekezi vya kubadilisha fedha za kigeni iliyotolewa leo Februari 10, 2022 na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Wakati huo huo, Euro ya Ulaya inanunuliwa kwa shilingi 2615.3 na kuuzwa kwa shilingi 2641.7.

Aidha,kwa mujibu wa BoT, Paundi ya Uingereza inanunuliwa kwa Shilingi 3105.8 huku ikiuzwa kwa Shilingi 3137.31.

Kwa upande wa Franka ya Rwanda inanunuliwa kwa shilingi 2.18 na kuuzwa kwa shilingi 2.245 huku shilingi ya Uganda ikinunuliwa kwa shilingi 0.624 na kuuzwa kwa shilingi 0.655.
Aidha, Randi ya Afrika Kusini inanunuliwa kwa shilingi 149.53 na kuuzwa kwa shilingi 150.99 huku shilingi ya Kenya ikinunuliwa kwa shilingi 20.14 na kuuzwa kwa shilingi 20.304.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news