Hazard aongoza ushindi wa Real Madrid

Winga wa Real Madrid, Eden Hazard amefunga bao lake la kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kujiunga na timu hiyo akitokea Klabu ya Chelsea siku za karibuni, anaripoti Mwandishi Diramakini.
Katika mtanange huo uliopigwa uwanja wa San Siro, Hazard amefunga bao hilo kwa mkwaju wa penalti dakika ya saba huku lile la pili likiwa ni la kujifunga kutoka kwa mchezaji wa Inter Milan, Achraf Hakimi dakika ya 59.

Aidha, Klabu ya Inter Milan ilikubali kufungwa mabao 2-0 ikiwa nyumbani katika uwanja huo na kuifanya ipoteze jumla ya mechi mbili na kuwa na sare mbili kati ya mechi nne ilizocheza ndani ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Katika msimamo wa kundi B, klabu hiyo ipo nafasi ya nne na Real Madrid wao wapo nafasi ya pili na alama zao wakiwa wamejikusanyia saba.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news