Mgogoro wa mpaka uliodumu kwa zaidi ya miaka 14 kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa na Wilaya ya Kilolo, unaohusisha vijiji vya Irole na Ilambilole, hatimaye umepatiwa ufumbuzi baada ya juhudi za pamoja za serikali.

Kamati za Ulinzi na Usalama za wilaya hizo, zikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Benjamini Sita, pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, zimefika katika eneo la tukio kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto hiyo iliyokuwa kikwazo kwa shughuli mbalimbali za maendeleo kwa wananchi.
Katika kikao kilichofanyika, wananchi kutoka pande zote mbili walipata nafasi ya kueleza malalamiko yao, huku wataalamu wa ardhi wakitoa ufafanuzi wa kitaalamu kuhusu mipaka halisi ya maeneo hayo.
Baada ya majadiliano ya kina, uamuzi wa mwisho kuhusu mpaka ulitolewa, hatua inayotarajiwa kumaliza sintofahamu iliyodumu kwa muda mrefu na kurejesha utulivu pamoja na ushirikiano kati ya wananchi wa vijiji hivyo.
Akizungumza mara baada ya kufikiwa kwa muafaka huo, viongozi wa wilaya hizo wamesisitiza umuhimu wa wananchi kuheshimu mipaka iliyowekwa ili kuepusha migogoro ya aina hiyo kujirudia.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo























